As we all know that Healthy matters,lets follow the readings for longevity of our lives now and then for sustainable healthy affairs

Tuesday, March 5, 2019

MATUMIZI YA VIUA VIJISUMU

Jinsi ya kutumia
Ifuatayo ni orodha ya dozi za amoksilini kwa njia ya mdomo, na ampisilini kwa njia ya sindano. Kila inapowezekana toa amoksilini kwa njia ya mdomo. Tumia ampisilini kwa njia ya sindano kwa magonjwa makali, au pale ambapo mtu anatapika au hawezi kumeza.

Kama ilivyo kwa dawa za antibiotiki zingine, muda wa kuendelea kutoa dawa hizo hutofautiana kutokana na sababu mbalimbali. Lakini kanuni ya msingi ni kuendelea kutoa dawa hadi dalili zote za maambukizi(ikiwemo homa) zitakapokuwa zimetoweka angalau kwa saa 24. Kwa watu wenye VVU, toa dawa kwa ajili ya siku zote zilizoorodheshwa. Vilevile, kuna kiwango kwa ajili ya kiasi cha dawa ambacho kinapaswa kutolewa. Kwa ujumla, toa kiasi cha chini kwa mtu mwembamba au kwa maambukizi yasiyo makali sana, na kiasi cha juu kwa mtu mwenye mwili mkubwa zaidi au dhidi ya maambukizi makali sana.

AMOKSILINI (MATUMIZI KWA NJIA YA MDOMONI)
Kwa maambukizi mengi miongoni mwa watoto
Toa miligramu 45 hadi 50 kwa kila kilo kwa siku, ikigawanywa katika dozi 2 kwa siku. Kama huwezi kumpima mtoto, mpe dozi kulingana na umri:
Chini ya miezi 3: toa miligramu 125, mara 2 kila siku kwa siku 7 hadi 10.
Miezi 3 hadi miaka 3: toa miligramu 250, mara 2 kila siku kwa siku 7 hadi 10.
Miaka 4 hadi 7: toa miligramu 375, mara 2 kila siku kwa siku 7 hadi 10.
Miaka 8 hadi 12: toa miligramu 500, mara 2 kila siku kwa siku 7 hadi 10.
Zaidi ya miaka 12: toa miligramu 500 hadi 875, mara 2 kila siku kwa siku 7 hadi 10.
Endelea kumpa amoksilini hadi angalau saa 24 baada ya dalili zote kutoweka.
AMPISILINI (KWA NJIA YA MDOMO)
Toa miligramu 50 hadi 100 kwa kila kilo kwa siku, ikigawanywa katika dozi 4 kwa siku. Kama huwezi kumpima mtoto, mpe dozi kulingana na umri:
Chini ya mwaka 1: toa miligramu 100, mara 4 kila siku kwa siku 7.
Mwaka 1 hadi 3: toa miligramu 125, mara 4 kila siku kwa siku 7.
Miaka 4 hadi 7: toa miligramu 250, mara 4 kila siku kwa siku 7.
Miaka 8 hadi 12: toa miligramu 375, mara 4 kila siku kwa siku 7.
Zaidi ya miaka 12: toa miligramu 500, mara 4 kila siku kwa siku 7.
Endelea kumpa ampisilini hadi angalau saa 24 baada ya dalili zote kutoweka.

AMPISILINI (KWA NJIA YA SINDANO)
Ampisilini inaweza pia kutolewa kwa njia ya sindano, lakini kwa magonjwa makali tu, au mahali ambapo mtu anatapika na hawezi kumeza.
Choma miligramu 100 hadi 200 kwa kilo, zikigawanywa katika dozi 4 kila siku. Kama huwezi kumpima mtu, mpe dozi kwa kuzingatia umri wake:
Chini ya mwaka 1: choma miligramu 100, mara 4 kila siku kwa siku 7.
Mwaka 1 hadi 5: choma miligramu 300, mara 4 kila siku kwa siku 7.
Miaka 6 hadi 12: choma miligramu 625, mara 4 kila siku kwa siku 7.
Zaidi ya miaka 12: choma miligramu 875, mara 4 kila siku kwa siku 7.
Erithromaisini (erythromycin)
Erithromaisini hufanya kazi dhidi ya maambukizi mengi yanayotibiwa na dawa zilizomo katika kundi la penisilini au tetrasaikilini, na inaweza kutumika kwa watu wanaopatwa na mzio kutokana na penisilini

No comments:

Post a Comment